Ushauri wa Kiusalama wa CPJ: Kuripoti kuhusu janga la virusi vya corona

Wanahabari nchini Mexico, wakiwa wamevalia vifaa kinga kutokana na janga la COVID-19, wakifuatilia maandamano ya wafanyakazi wa huduma za usimamizi katika Hospitali ya Balbuena, Jiji la Mexico mnamo Aprili 16, 2020. (AFP/Pedro Pardo)

Imebadilishwa mara ya mwisho Mei 20, 2021

Shirika la Afya Duniani (WHO) liliutangaza mlipuko wa ugonjwa wa virusi vya COVID-19 (maarufu pia kama virusi vipya vya corona) kuwa ulioenea kote duniani, yaani pandemic mnamo Machi 11, 2020. Hali duniani inaendelea kubadilika, na mataifa yanaongeza au kulegeza vikwazo vya usafiri na/au hatua nyingine za kujikinga huku aina mpya za virusi vya corona zikiendelea kutambuliwa na mipango ya kuwapa watu chanjo ya COVID-19 kushika kasi, kwa mujibu wa ripoti za vyombo vya habari.

Wanahabari kote duniani wanatekeleza jukumu muhimu katika kuufahamisha umma kuhusu virusi hivi na juhudi za serikali za kukabiliana na virusi hivyo. Hii ni licha ya majaribio ya serikali katika mataifa kadha kudhibiti uhuru wa kuripoti na kupata habari, kama ilivyonakiliwa na CPJ. Wanahabari wanakabiliwa na shinikizo kubwa na mara kwa mara wanakuwa hatarini ya kuambukizwa kupitia kusafiri, kufanya mahojiano, na pia katika maeneo ambayo wanafanyia kazi, kwa mujibu wa mahojiano ya CPJ na wanahabari. Wanahabari wamezuiwa kutoa habari, kuzuiliwa, kushambuliwa kimwili na mtandaoni, na kupoteza mapato kutokana na COVID-19, kama ilivyoangaziwa katika ripoti za hivi karibuni za CPJ.

Ili kufahamu ushauri wa karibuni zaidi na masharti yanayowekwa, wanahabari wanaoripoti kuhusu mlipuko huu wanafaa kufuatilia taarifa kutoka kwa WHO na za mamlaka za afya nchini mwao.

Kwa maelezo ya karibuni zaidi kuhusu mlipuko huu, Kituo cha Habari Kuhusu Coronavirus cha Chuo Kikuu cha John Hopkins ni chanzo salama na cha kutegemewa.

Kujiweka salama ukiwa kazini kuripoti

Marufuku dhidi ya usafiri wa kimataifa na/au hatua nyingine za kuzuia kusambaa kwa maambukizi zinabadilika mara kwa mara. Hii ina maana kuwa kazi za kuripoti, zinaweza kubadilika kukiwa na ilani ya muda mfupi au bila notisi yoyote.

Wahudumu wa vyombo vya habari ambao wamepewa chanjo wanafaa kutambua kuwa bado wanaweza kusambaza virusi hivyo, kwa mujibu wa Kituo cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa cha Marekani (CDC), na kwamba chanjo mbalimbali hutoa viwango tofauti vya kinga dhidi ya aina tofauti za virusi hivyo, kwa mujibu wa Yale Medicine. Hatua za kujiweka salama dhidi ya COVID-19, kama vile kukaa umbali na kuvalia barakoa, kwa hivyo zinafaa kuendelea kuzingatiwa.

Wanahabari wanaopanga kuripoti kuhusu janga la COVID-19 wanafaa kuzingatia ushauri ufuatao kuhusu usalama wao:

Kabla ya kwenda kuripoti

Afya ya kiakili

Kujikinga dhidi ya Maambukizi & Kuwaambukiza wengine

Mataifa mengi yanaendelea kutekeleza ushauri wa watu kutokaribiana, ingawa umbali unaohitajika unaweza kuwa tofauti kwa kutegemea taifa husika. Iwapo unatokea eneo lenye hatari kubwa ya kuambukizwa, kama maeneo yafuatayo hapa chini, uliza awali kuhusu hatua za usafi na usalama ambazo zinatekelezwa humo. Ukiwa na shaka zozote, usizuru:

Ushauri wa kawaida wa kujikinga na maambukizi

Vifaa vya Kukinga Mwili (PPE)

Kwa kutegemea kazi yako ya kuripoti ni ya aina gani, waandishi na wahudumu wengine vya vyombo vya habari wanaweza kuhitajika kuvalia vifaakinga au PPE za kimatibabu za aina mbalimbali. Hizi zinaweza kuwa kwa mfano glavu za kutupwa baada ya kutumiwa, barakoa au mask, aproni za kujikinga/ovaroli/ vazi maalum la kukinga mwili dhidi ya maambukizi linaloufunika mwili wote, na vifunikia viatu na kadhalika.

Kuvalia na kuvua vifaa kinga vyovyote vile kwa njia salama ni jambo linalohitaji mtu kufuata ushauri wa kiusalama kwa umakinifu. Tafadhali bofya hapa kusoma ushauri kutoka kwa CDC. Unafaa kuwa makini zaidi unapovua vifaakinga, kwani wakati huo ndio hatari ya kuambukiza ilipo juu zaidi. Iwapo una shaka, tafuta ushauri wa wataalamu na upokee mafunzo kabla ya kwenda kazi yoyote ile kuripoti

Fahamu kuwa katika baadhi ya mataifa kunaweza kuwa na uhaba wa vifaakinga vya kimatibabu vilivyo bora na hivyo basi ni vigumu kupata vifaa hivyo, kwa hivyo kuvitumia kunaweza kuchangia uhaba zaidi.

Barakoa au mask

Kutumia mask au barakoa ipasavyo ni muhimu sana kwa wahudumu wa vyombo vya habari wanaoripoti kutoka maeneo yenye watu, kwenye maeneo yaliyofungana, na/au katika maeneo yenye hatari zaidi ya kuambukizwa. Unafaa kufahamu kwamba kiwango cha matone yenye virusi hewani katika maeneo yenye watu wengi au yasiyo na mtiririko mzuri wa hewa kinaweza kuwa cha juu kuliko kawaida, na hivyo hilo linaweza kuongeza hatari ya kuambukizwa.

Fahamu kuwa zisipotumiwa vyema, kuna wasiwasi kwamba barakoa zinaweza kuwa chanzo cha maambukizi. Utafiti wa Lancet unaonyesha kulikuwa na masalio ya virusi kwenye barakoa ya kimatibabu kufikia siku saba baada ya kuwa kwenye eneo lenye virusi. Kwa kuzingatia utafiti huu, kuvua au kutumia tena barakoa, au kuugusa uso wako unapokuwa umevalia mask kunaweza kukuweka hatarini ya kuambukizwa.

Iwapo utavalia barakoa, unafaa kufuata ushauri ufuatao:

Usalama wa Vifaa

Kuna hatari ya kusambazwa kwa COVID-19 kupitia vifaa na mitambo iliyoambukizwa. Vifaa vyote vinafaa kuoshwa vyema na kutakaswa wakati wote:

Kuvisafisha Vifaa vya Kielektroniki

Hapa chini tumeorodhesha baadhi ya mambo unayoshauriwa kuzingatia kwa kawaida wakati wa kuvisafisha vifaa vyako vya kielektroniki. Hakikisha kila wakati kwamba umesoma mwongozo wa mtengenezaji wa kifaa kabla ya kujaribu njia yoyote ya kukisafisha.

Unaweza kupata ushauri zaidi na wa kina kupitia taarifa hii.

Usalama wa kidijitali

Uhalifu & usalama wako ukiwa kazini kuripoti

Kwenda kuripoti nje ya nchi

Kutokana na marufuku na vikwazo vya usafiri vilivyotolewa na mataifa mengi duniani, inaendelea kuwa vigumu kusafiri nje ya nchi. Hata hivyo, iwapo inawezekana kwenda kuripoti nje ya nchi yako, unafaa kuzingatia yafuatayo:

Baada ya kuripoti

–Iwapo una dalili za kuugua

Kifurushi cha Usalama cha CPJ kinawapa wanahabari na mashirika ya habari maelezo mengi ya msingi kuhusu usalama wa wanahabari kikiangazia mwili, akili na dijitali, na pia kinaangazia jinsi ya kuripoti kuhusu fujo za raia na uchaguzi.

[Angalizo la mhariri: Ushauri huu ulichapishwa mara ya kwanza mnamo Februari 10, 2020, na unafanyiwa mabadiliko mara kwa mara. Tarehe ya kuchapishwa inayoonyeshwa pale juu inaonyesha tarehe ya karibuni zaidi ya mabadiliko.]

Exit mobile version